Back to top

MOI kuanza kupasua Ubongo bila ya kufumua fuvu la kichwa

22 November 2019
Share

Taasisi  ya  mifupa  MOI  imeanza   kufanya  upasuaji  wa  Ubongo  bila  ya  kufungua  fuvu  la   kichwa  ambapo  upasuaji huo unafanyika  kwa kutumia  mishipa ya damu pekee ambapo kuazia  Januari mwakani huduma hizo  zitapanuka zaidi  hata kwa  wagonjwa  kutoka  nje  ya  nchi.

Hayo  yamesemwa  na  mkurugenzi  mtendaji  wa   MOI Dkt. Respicious   Bonifas  wakati  akizungumza kuhusu Utekelezaji  wa shughuli mbalimbali   za  taasisi hiyo  kwa kipindi cha miaka minne.