Waziri wa madini Mhe.Dotto Biteko amemsimamisha kazi afisa madini mfawidhi mkoa wa Arusha Robert Erick kwa uzembe wa kushindwa kusimamia wafanyabiashara wa madini kuingia kwenye soko la madini na kusababisha wafanyabiashara kuendelea kutorosha madini huku akiagiza wafanyabiashara wote wawe wameamia kwenye soko hilo hadi ifikapo jumatatu ya wiki ijayo
Mhe.Dotto Biteko ametoa maamuzi hayo alipofanya ziara kwenye soko la madini la mkoa wa Arusha na kugundua mapungufu hayo
Awali katibu mkuu wizara ya madini Prof.Simon Msanjila alieleza masikitiko yake kuhusu hali hiyo huku wafanyabiashara wa madini wakawakilisha changamoto zinazowakabili.