Wizara ya Afya imewasilisha vipaumbele 11 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI ambavyo ni pamoja na kuimarisha huduma za kinga dhidi ya magonjwa ya mlipuko na magonjwa yasiyoambukiza, kuimarisha upatikanaji na ubora wa huduma za afya zinazotolewa kwenye ngazi za msingi hadi Taifa.