Back to top

MAFUNZO KWA ASKARI WA KIKE AFRIKA YAFUNGULIWA ABUJA NIGERIA.

02 July 2024
Share

Mafunzo kwa Askari wa kike ukanda wa Afrika (IAWP) yamefunguliwa leo katika kituo cha Rasilimali ya Polisi Abuja Nchini Nigeria ambapo mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo askari wa kike ukanda wa Afrika na wasimamizi wa sheria.

Akiongea Jijini Abuja Nchini Nigeria katika ufunguzi wa mafunzo hayo Rais wa shirikisho la askari wakike Duniani Dkt.Leah Shibambo’s ameshukuru shirikisho la wakuu wa Polisi kwa namna ambavyo wakuwa na agenda za kuongeza nafasi za wanawake katika ajira na mgawanyo wa majukumu.

Ameongeza kuwa kitendo cha wakuu hao wa Polisi kuwa na agenda za kuwaweza na kujengea uwezo wanawake imeongeza kujiamini kwa kundi hilo katika utekelezaji wa majukum yao  huku ikileta matokeo Chanya katika kutoa huduma bora katika jamii.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Nigeria IGP Phd Kayode Egbetokun amesema kuwajengea uwezo askari wakike umewasaidia na kufanya askari hao kujituma katika kazi na  kujiamini kitendo kilicholeta matokeo Chanya katika jamii huku akibaisha kuwa mafunzo hayo yamekuja wakati sahihi  ambapo dunia imejikita katika usawa wa kijinsia.

Kamishna Msaidizi mwandamizi wa Polisi kutoka Nchini Tanzania Dkt SACP Debora Magiligimba ambaye ni mjumbe kutoka Tanzania anayeongoza Kanda ya ishiriki na moja ya nchi za SADC amebainsha kuwa mafunzo hayo yanakwenda kuongeza ufanisi katika kazi zao za kila siku.

Mrakibu wa Idara ya Uhamiaji kutoka Nchini Ghana SI Doris Hajiman amebainisha kuwa maandalizi ya mafunzo hayo ni mazuri huku akiwapongeza waandaji wa mafunzo hayo ambao Nchi ya Nigeria.