Back to top

Corona: DC Simalenga atishia kupiga stop minada, magulio na masoko.

07 August 2021
Share

Mkuu  wilaya ya Songwe Bw.Simon Simalenga ametishia kusitisha vibali vya shughuli za minada, magulio na masoko kwa muda usiojulikana iwapo wananchi wataendelea kupuuza maelekezo ya kujihadhari na janga la Covid-19 na kwamba suala la uvaaji barakoa, kunawa mikono kwa maji tiririka na kuepuka misongamano ni la lazima kutekelezwa.
.
Bw. Simalenga amesema halidhishwi na mwenendo wa wananchi katika kuzingatia taratibu zilizowekwa na serikali katika kukabiliana na virusi vya corona kwenye maeneo ya mikusanyiko, misongamano, mikutano na misiba. 
.
Aidha Mkuu huyo wa wilaya amesema,  kutokana na hali hiyo baadhi ya vibali havitatolewa kuanzia juma lijalo mpaka serikali itakapojiridhisha kuwa hali ya tahadhali hizo imeimarika.