Back to top

DC SIMALENGA AAGIZA WAZAZI WANAOSHAWISHI UTORO  KUCHUKULIWA HATUA.

14 January 2023
Share

Mkuu wa wilaya ya Songwe Simon Simalenga ,amewaagiza  watendaji wa vijiji na kata katika tarafa ya Kwimba, kuwachukulia hatua kali baadhi ya wazazi kutoka jamii za wafugaji, wakulima na wavuvi, ambao wanadaiwa kuwashawishi wanafunzi wanaotakiwa kuanza darasa la kwanza na kidato cha kwanza  kutoripoti shuleni, na badala yake kuwatumia katika shughuli zao, hali inayosababisha zoezi la kuripoti kwa wanafunzi hao kusuasua.

Dc Simalenga ametoa maagizo hayo wakati akizungumza na walimu wakuu, watendaji wa vijiji  na kata kutoka tarafa hiyo .