Back to top

Sheria mpya ya uchaguzi yapitishwa Zanzibar .

17 December 2019
Share

Tume ya uchaguzi ya Zanzibar imepitisha sheria  mpya ambapo kwa mara ya kwanza uchaguzi mkuu  kwa upande wa Zanzibar  baadhi ya wadau wataruhusiwa kupiga kura siku moja kabla ya siku yenyewe.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti  wa Tume ya uchaguzi ya Zanzibar Jaji mkuu Mstaafu Hamid Mahmud wakati akizindua sheria hiyo kwa viongozi wa vyama vya siasa 19 na wadau wa sekta za jamii katika mkutano wa pamoja  ambapo amesema  kwa kuanzia  utaratibu huo ni watendaji wa tume na  askari watakaohusika na ulinzi na usalama wa siku ya upigaji kura.