Back to top

RC MAKONGORO ASIMULIA MAKUBWA YA MAMA SAMIA LEGAL AID

25 February 2025
Share

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Charles Makongoro Nyerere ametoa pongeza kwa timu za uratibu wa kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kufuatia utatuzi wa migogoro unaofanywa na timu hizo

Mhe. Makongoro amesma kuwa wakati akiwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara ambapo kampeni hiyo ilipita aliwakutanisha wataalamu wa sheria na wananchi wanne ambao baadae walimpa mrejesho kuwa changamoto zao zilipata majibu.

Hatahivyo ametumia fursa hiyo kuwasihi wananchi wa Mkoa wa Rukwa kujitokeza kwa Wingi katika kampeni hiyo ili changanoto zao za Kisheria ziweze kupatiwa ufumbuzi.