Back to top

EMMANUEL TUTUBA BOSI MPYA BOT

08 January 2023
Share

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan, amemteua Bw.Emmanuel Mpawe Tutuba, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Bw.Tutuba anachukua nafasi ya Prof. Florens Luoga ambaye amemaliza kipindi chake.

Aidha Rais Samia amemteua Dkt.Natu El- Maamry Mwamba kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango.

Dkt.Mwamba alikuwa Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Uendeshaji wa Kiwanja cha Ndege cha Kilimanjaro (KADCO).

Dkt.Mwamba anachukua nafasi ya Bw.Emmanuel M.Tutuba ambaye ameteuliwa kuwa Gavana wa Benki Kuu.

Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imeeleza kuwa uteuzi huo unaanza mara moja.