Back to top

KIGOGO DAWA ZA KULEVYA AKAMATWA MAREKANI

26 July 2024
Share

Mmoja wa wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya, Ismael "El Mayo" Zambada, Kiongozi wa genge la Sinaloa la Mexico, amekamatwa na Maajenti wa Shirikisho la Marekani huko El Paso, Texas.

Mnamo Februari Mwaka huu, Zambada alishtakiwa na waendesha mashtaka wa Marekani kwa njama ya kutengeneza na kusambaza , dawa yenye nguvu zaidi kuliko heroini ambayo imekuwa imelaumiwa na Marekani.