Back to top

ANASA AKIOKOA SIMU YAKE KWENYE MIAMBA.

23 October 2024
Share

Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Matilda Campbell, yalimkuta makubwa wakati akijaribu kuokoa simu yake iliyoangukia katikati ya miamba baada ya kunasa kichwa katikati ya mawe mawili huku miguu yake ikibaki inaning'inia juu na kushindwa kujiokoa huko New South Wales Hunter Valley huko nchini Australia.


Matilda Campbell, kutoka Newcastle, NSW, alinaswa kwenye shimo lenye umbo la S, baada ya kudondosha simu yake alipokuwa akitembea kichakani na marafiki zake katika Bonde la Hunter ambapo picha za tukio hilo hazikuonyesha chochote zaidi ya miguu ya Bi Campbell alipokuwa akining'inia kichwa chini miguu juu.

Wenzake walipambana kumuokoa bila mafanikio katika shimo hilo la mita tatu kwa takriban saa moja, kabla ya kuita huduma za dharura kuja kumuokoa.


Matilda alifanikiwa kuokolewa na timu iliyoongozwa na daktari wa dharura Peter Watts ambaye alijenga fremu ya mbao kuzunguka eneo hilo ili kushikilia mawe makubwa nje ya njia, na baada ya tukio hilo Matilda alichapisha picha zake za tukio mtandaoni zilizoambatana na ujumbe wa kukishukuru kikosi hicho.