![](https://www.itv.co.tz/sites/default/files/styles/large/public/field/image/al.jpg?itok=iE3ZtLH7)
Mwongozaji wa kifaa cha kunyanyulia mizigo (Crane Lift) kinachotumika katika ujenzi wa daraja la Magufuli Kigongo-Busisi anahofiwa kufariki dunia baada ya kifaa hicho kuacha njia na kutumbukia katika Ziwa Victoria ambapo juhudi za uokoaji zinaendelea zikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel pamoja na vikosi vya uokoaji.