Back to top

TPA yashauriwa kuangalia upya gharama za usafirishaji Mtwara.

30 October 2018
Share

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa amesema kuna haja ya  Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kuziangalia upya gharama  za usafirishaji katika bandari ya Mtwara,  kwani ni kubwa na hivyo kusababisha  meli ya wafanyabiashara kutoka nchini Comoro kusitisha biashara na Tanzania.

Akaongeza kuwa wafanyabiashara wote wataikimbia bandari hiyo lakini pia athari yake ni kubwa kwa  uchumi wa mkoa na taifa kwa ujumla.