Back to top

Wananchi Njombe wapongeza kukamatwa kwa watuhumiwa 28 wa mauaji.

04 February 2019
Share

Baadhi ya wananchi kutoka kata ya Mjimwema  wilayani Njombe mkoani Njombe ,wameelezea kuridhishwa na ukamatajwa wa watuhumiwa 28 wa mauaji ya watoto wilayani humo  katika oparesheni inayoondeshwa na kikosi utendaji cha operasheni na mafunzo cha Jeshi la polisi huku wakiwaomba wenzio wasijichukulie sheria mkononi kukabiliana na tatizo hilo.

Siku za hivi karibuni kumejitokeza aina nyingine ya mauaji ya watu watatu yanayodaiwa kutekelezwa na wananchi kwa kujichukulia sheria mkononi na  kuwaua watu wanaohisiwa au kutuhumu kuwa huenda ndio vinara wanaotekeleza matukio ya utekeji na kuwaua watoto.