Back to top

Likizo za lazima zaanza Zanzibar.

05 April 2020
Share

Katika harakati za kupambana na maambukizi ya virusi vya corona serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeridhia kwa baadhi ya taasisi zake kutoa likizo za lazima ili kupunguza msongamano  na mikusanyiko maofisini.

Habari ambazo ITV imezipata tayari baadhi ya wizara  za serikali zimeanza utaratibu wa kuwapa likizo za lazima  wafanyakazi  huku baadhi ya mashirika wafanyakazi  wakibadilishana na wenzao baada ya siku kumi huku Mfanyakazi wa ZSTC Ali Meraji amekiri kupewa agizo la kubaki nyumbani.