Back to top

MWAMPOSA AKOSHWA NA UWEKEZAJI IPP MEDIA

23 July 2024
Share

Mtume na Nabii Boniface Mwamposa (Buldoza) wa Kanisa la Arise and Shine, (Inuka Uangaze) ametembelea Kampuni ya IPP Media na Kupokelewa na Mwenyeji wake, Mkurugenzi Mtendaji wa ITV/Radio, Joyce Mhaville, ambapo amepongeza shughuli zinazofanywa na vituo hivi za kuhabarisha umma huku akikoshwa na uwekezaji mkubwa uliopo. 

Ujio wa Mwamposa, ITV/Radio One, Capital Radio na Capital TV, ulikuwa umeongozana na jopo la wasaidizi wake kutoka Kanisa la Arise and Rise, lililopo Kawe, Dar es Salaam, akiwemo Askofu Jacob Mwakibinga na John Ssekelala.

Pia viongozi wa ITV/Radio One na Capital TV/Radio, Deogratius Rweyunga (Mkurugenzi Radio One), Pius Paul (Mkurugenzi wa ITV na Capital TV) na Steven Chuwa (Mhariri ITV), walipata nafasi ya kumtembeza ndani ya kituo hiki, kuona namna Maandalizi ya Habari na vipindi mbalimbali vinavyo andaliwa ili kuufikia Umma wa Watanzania kwa kuzingatia misingi ya taaluma ya habari.