
Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassani amezindua kikosi kazi kitakachofanya kazi ya kutatua changamoto za viumbe vamizi ambavyo vinatajwa kuwa ni janga kwa Taifa kwa sasa.
Amesema Tanzania ina viumbe vamizi zaidi ya 100 hivyo lazima hatua za haraka zichukuliwe kuvikabiliwa huku akiwataka wataalam kufanya kazi zinazoonekana katika jamii badala ya kutoa majina ya kisayansi tu ya vimumbe hao.